Wekeni kipaumbele habari za uchunguzi sekta ya bima na Mamlaka itatoa ushirikiano – Dkt. Saqware
Hayo yamesemwa na Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware katika kikao kazi na wahariri, pamoja na waandishi wa habari kuhusu bima ya afya kwa wote kilichofanyika Februari 2, 2026 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo ametoa msisitizo kwa wanataaluma hiyo kutumia kalamu zao vizuri katika kuandika habari za kiuchunguzi ndani ya sekta ya bima.
Kamishna pia alisisitiza Mamlaka itatoa ushirikiano thabiti ukiwemo wa kifedha katika kufanikisha kazi hizo za kiuchunguzi ambazo pia zitakuwa chachu za kuibua udanganyifu katika bima na kuimarisha soko la bima.
Mgeni rasmi katika kikao kazi alikuwa Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa, pia kilihudhuriwa na Taasisi nyingine kama NHIF, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete na wadau wengine mbalimbali.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA
