Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
TIRA yatoa elimu ya bima katika maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano Zanzibar
23 Apr, 2026
TIRA yatoa elimu ya bima katika maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano Zanzibar

Zanzibar, Aprili 23, 2026 — Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya bima ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayoendelea Mjini Magharibi, Zanzibar.

TIRA tunapatikana katika banda maalum mkabala na Banda la Benki Kuu kwenye Uwanja wa Mao Zedong, ambapo wananchi na wageni wanaotembelea maonesho hayo wanapata fursa ya kujifunza kuhusu umuhimu wa Bima, namna inavyofanya kazi, pamoja na faida zake katika kulinda maisha na mali.

Akizungumza na wanahabari katika banda hilo, Meneja wa TIRA - Kanda ya Unguja, Ndugu Kurenje Mbura, amewahimiza wakaazi wa Zanzibar pamoja na wageni kutoka Tanzania Bara na maeneo mengine kutembelea banda la TIRA ili kupata elimu sahihi kuhusu huduma za bima.

Amesema elimu hiyo ni muhimu katika kuongeza uelewa wa jamii na kuhamasisha matumizi ya huduma za bima kama njia ya kukabiliana na majanga na hatari mbalimbali.

Maadhimisho hayo yalianza Aprili 21, 2026 na yamezinduliwa rasmi na Waziri wa Kazi na Uwekezaji - Zanzibar Mhe. Shariff A. Shariff, huku yakitarajiwa kufikia tamati Aprili 27, 2026.

TIRA, Kwa Soko Salama la Bima