Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
TIRA yashiriki kikao kazi kuhusu Utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote (UHI) na APHTA
10 Feb, 2026
TIRA yashiriki kikao kazi kuhusu Utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote (UHI) na APHTA

 

Leo Februari 10, 2026 TIRA imeshiriki kikao maalum ambacho kimejadili masuala muhimu kuhusu bima ya afya kwa wote.  Kikao hicho kimeandaliwa na Wizara ya Afya na kuongozwa na Mgeni Rasmi; Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekilaghe lengo likiwa ni ushirikishwaji wa wadau katika utekelezaji wa UHI ambapo mazungumzo yamefanyika na Umoja wa Wamiliki wa Watoa Huduma za Afya za Binafsi (APHTA), Crown Plaza, jijini Dar es Salaam.

Aidha, kikao hicho kimehudhuriwa na Taasisi mbalimbali kama NHIF, UNDP na GIZ  ambapo kimekuwa na manufaa makubwa katika utekelezaji wa UHI kwa kujadili mchango wa wadau mbalimbali katika kufikia lengo la upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi. TIRA ilipata fursa ya kuelezea majukumu yake ya usimamizi, sheria na kanuni zake katika jukumu hilo.

APHTA wametoa maoni mbalimbali ambayo yamelenga kushirikiana na Serikali katika utekelezaji huo na Katibu Mkuu Dkt. Shekilaghe amewapongeza kwa dhamira yao njema  na kueleza  Wizara imejipanga vyema kwa kushirikiana na wadau pia  amesisitiza Serikali ni sikivu na ipo tayari kupokea maoni mbalimbali katika utekelezaji wa UHI.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA