Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
TIRA yaratibu tamasha la michezo Arusha, Elimu ya bima yatolewa
22 Mar, 2026
TIRA yaratibu tamasha la michezo Arusha, Elimu ya bima yatolewa

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA) Kanda ya Kaskazini hapo jana Machi 21, 2025 imeratibu na kushiriki tamasha kubwa  la elimu ya bima na michezo katika Chuo cha Uhasibu Arusha kwa lengo la kujengea uwezo kuhusu maswala ya bima ambapo zaidi ya wanafunzi mia tatu wamehudhuria tamasha hilo.

Akizungumza kwenye hafla hiyo jijini Arusha Meneja wa Kanda ya Kaskazini Dkt.  Emmanuel Lupilya amesema kuwa, kupitia tamasha hilo wanafunzi hao wameweza kupata elimu kuhusu maswala mbalimbali ya Bima  na kuweza kuzijua faida za kukata bima mbalimbali.

Dkt. Lupilya amewaasa wanafunzi waliopo vyuo mbalimbali nchini kuhakikisha swala la bima haliepukiki kwani ndio uti wa mgongo  katika kuhakikisha uchumi unajengwa sio tu kwa fedha bali kwa misingi ya kuwekeza kwenye bima kukinga mali afya pamoja na jamii yote kwa ujumla wake.

“Jamii inayofundishwa na kuelimishwa juu ya elimu ya bima hakika serikali yake haiwezi kubeba mzigo mzito wa majanga hivyo tunahamisha hayo majanga kuelekea kwenye makampuni ambayo tunayasajili sisi kama mamlaka ili kuona kuwa shughuli zote za uchumi kijamii zinazoendeshwa na wananchi zinaenda kukingwa na bima .”amesema Dkt.Lupilya.

Amesema kuwa  ,TIRA ipo kwa ajili ya kukinga ndoto za wadau wote wakiwemo  jamii,wanafunzi ,na ndicho kimewafanya kufika chuoni hapo  kutoa elimu upande wa bima na michezo ili michezo iwaandae vijana hawa kuwa wabunifu na weledi katika maswala ya kuonesha ukomavu kwenye uongozi kwa baadaye .

“Tumeanza leo kwenye chuo cha uhasibu Arusha lakini ndoto zetu ni kufika mikoa na wilaya zote ambazo tunazisimamia kupitia Kanda hii ya Kaskazin .”amesema .

Aidha, ametaja matarajio  yao ya baadaye ni kufikia walengwa zaidi hususani jamii ambayo haijafikwa na bima na kuweza kufika  vijijini na hata maeneo ambayo wanananchi wanahitaji huduma hiyo ya bima .

“Tumepanga utaratibu wa kuwafungulia wakala ambao utakuwa ni shirikishi kwa maana ya chuo wanakuwa na uwakala ili shughuli zote za kusimamia maswala ya kijamii katika chuo hiki ziweze kufanikiwa, tutahakikisha makampuni yetu yanatengeza bidhaa ambazo zinajibu changamoto ambayo imekuwa kubwa katika nchi yetu na kuondokana na utegemezi kuomba fedha kila wakati na kuona namna ambavyo bima itasaidia nchi na kusonga mbele na kuhakikisha ndoto za hawa wanafunzi zinafikiwa .”amesema Dkt.Lupilya.

Nao baadhi ya wanafunzi walioshiriki tamasha hilo, Abdalah Juma na Jenifa Jeremiah wamesema kuwa kitendo kilichofanywa na TIRA ni mfano wa kuigwa naTaasisi na Makampuni  mengine kwani wameweza kuwajengea uelewa mkubwa kuhusu maswala ya bima na kuahidi kubwa mabalozi wazuri wa kwenda kutangaza elimu hiyo popote watakapokuwa.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA