TIRA tunashiriki kikao kazi na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu bima ya afya kwa wote
Wizara ya Afya leo imeandaa kikao maalum cha wahariri wa vyombo vya habari katika Ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujadili utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote na nafasi ya vyombo vya habari katika kuelimisha jamii kuhusu mpango huo wa kitaifa.
Kikao hicho kitaongozwa na Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi, na kimewakutanisha wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari pamoja na wadau muhimu wa sekta ya afya na bima ambapo TIRA itawakilishwa na Kamishna wa Bima, Kurugenzi ya Bima ya Afya kwa Wote, Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima (TIO), Kurugenzi ya Sheria, Ofisi ya Kanda ya Mashariki,Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma na taasisi nyingine zinazohusika na utoaji na usimamizi wa huduma za bima ya afya.
