The United Republic of Tanzania

Tanzania Insurance Regulatory Authority

“TIRA kwa Soko Salama la Bima”
TIRA, PDPC zaimarisha ushirikiano kulinda taarifa binafsi
16 Sep, 2026
TIRA, PDPC zaimarisha ushirikiano kulinda taarifa binafsi

TIRA, PDPC zaimarisha ushirikiano kulinda taarifa binafsi

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) tarehe 15 Septemba 2026, imepokea timu ya viongozi na wataalamu kutoka Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu Dar es Salaam, katika ziara iliyolenga kuimarisha ushirikiano na uelewa wa pamoja kuhusu ulinzi na usalama wa taarifa binafsi katika sekta ya bima.

Ziara hiyo imekuwa fursa kwa TIRA na PDPC kubadilishana uzoefu na kujadili namna bora ya kuhakikisha taarifa binafsi zinazokusanywa na kuchakatwa katika utekelezaji wa majukumu ya TIRA zinatumika kwa usahihi, usalama na kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Aidha, Bi. Khadija Said; Naibu Kamishna wa Bima ameeleza kuwa TIRA itaendelea kushirikiana na PDPC katika kuimarisha ulinzi na usalama wa taarifa binafsi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha utawala bora, uwajibikaji na uaminifu katika sekta ya bima. 

Ushirikiano huo pia unalenga kuhakikisha taarifa binafsi za wananchi na wadau wa sekta ya bima zinashughulikiwa kwa umakini na kwa kuzingatia matakwa ya kisheria.

TIRA, Kwa Soko Salama la Bima