The United Republic of Tanzania

Tanzania Insurance Regulatory Authority

“TIRA kwa Soko Salama la Bima”
TIRA na Congo zakutana Lake Tanganyika Expo 2026, Bima za Baharini zatajwa
20 Sep, 2026
TIRA na Congo zakutana Lake Tanganyika Expo 2026, Bima za Baharini zatajwa

Waziri wa Jimbo la Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo upande wa Nishati na Madini; Mataka Mufwa leo Septemba 19, 2026 ametembelea banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) katika Maonesho ya Lake Tanganyika Expo 2026 yanayoendelea mkoani Kigoma, ambapo amepata elimu kuhusu majukumu ya Taasisi hiyo katika kusimamia na kuendeleza sekta ya bima nchini.

Aidha, Mhe. Mataka Mufwa ameeleza umuhimu wa Tanzania na Congo kushirikiana katika kuimarisha matumizi ya bima za baharini, hususan katika shughuli za usafirishaji na biashara zinazofanyika katika Ziwa Tanganyika.

Amebainisha kuwa ushirikiano huo unaweza kusaidia kuwakinga wananchi dhidi ya athari za ajali za majini, zikiwemo ajali za moto kwenye vyombo vya usafiri majini na kuzama kwa vyombo hivyo, ambazo zinaweza kusababisha upotevu wa maisha na mali. Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uelewa kuhusu bima za baharini ili kusaidia kulinda watu na mali zao pamoja na kupunguza athari za kiuchumi zinazotokana na majanga hayo.

Kwa upande wake; Meneja wa TIRA Kanda ya Ziwa Tanganyika Bw. Joel Ahaz amesema TIRA itaendelea  kushirikiana nchi za kanda ya Ziwa hilo katika kuhakikisha wananchi wanakingwa na bima pamoja na mali zao.

TIRA, kwa Soko Salama la Bima