TIRA Kanda ya Ziwa yaendelea kutoa mafunzo kwa watoa huduma za bima
17 Feb, 2026
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania Kanda ya Ziwa, imewataka mawakala wa bima kuongeza juhudi katika kuwafikia wananchi wengi zaidi ili kukuza uelewa na matumizi ya huduma za bima.
Akizungumza katika kikao cha mafunzo ya mawakala wa kampuni ya Bima ya Heritage kilichofanyika jijini Mwanza, Kaimu Meneja -TIRA Bw. Oyuke Phostine, alisema sekta ya bima ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa taifa na ustawi wa jamii, hivyo ni muhimu kila wakala kutimiza wajibu wake kwa weledi na uadilifu.
Bw. Oyuke alisisitiza kuwa bado kuna idadi kubwa ya wananchi katika Kanda ya Ziwa ambao hawajafikiwa na huduma za bima kutokana na ukosefu wa elimu na taarifa sahihi.
