Siku ya Zanzibar Saba Saba 2026, yafungua fursa za biashara na uwekezaji
Siku ya Zanzibar Saba Saba 2026, yafungua fursa za biashara na uwekezaji
Leo Juni 12, 2026 Maonesho ya kimataifa ya Biashara Saba Saba 2026 yamefana kwa uwepo wa ‘Siku ya Zanzibar’ ambayo imefungua majadiliano ya fursa za biashara na uwekezaji kwa washiriki na wadau wa Maonesho hayo ambapo TIRA imeshiriki.
Aidha, Siku ya Zanzibar imefunguliwa rasmi na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Ayoub Mohammed (MB) ambaye amesisitiza matumizi ya fursa za biashara, utalii na uchumi wa buluu ambapo pia Mfuko wa Bima ya Afya Zanzibar (ZHSF) wametoa wasilisho linaloeleza mipango mikakati ya kuimarishwa kwa mfuko huo ili kila mwananchi anufaike na huduma za bima.
TIRA imewakilishwa na Naibu Kamishna Bi. Khadija I. Said ambaye ameungana na viongozi mbalimbali kuadhimisha siku hiyo.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA
