Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Mkutano wa Wanawake Sekta ya Fedha: Kamishna wa Bima atoa rai kutengenezwa bidhaa za bima mahsusi kwa Wanawake 
23 Mar, 2026
Mkutano wa Wanawake Sekta ya Fedha: Kamishna wa Bima atoa rai kutengenezwa bidhaa za bima mahsusi kwa Wanawake 

Mkutano wa Wanawake Sekta ya Fedha: Kamishna wa Bima atoa rai kutengenezwa bidhaa za bima mahsusi kwa Wanawake 

Dkt. Baghayo Saqware; Kamishna wa Bima ametoa rai hiyo leo Machi 23,2026, kwa wanawake wanaoshiriki Mkutano wa Wanawake Sekta ya Fedha na kusisitiza Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) ipo tayari kupokea na kuthamini bidhaa mbalimbali za bima mahsusi kwa ajili ya wanawake ili kuongeza wigo wa bidhaa hizo katika soko la bima. Mkutano huo unaendelea jijini Arusha, katika ukumbi wa PAPU Tower. 

Dkt. Saqware kama mgeni mualikwa na mzungumzaji wa jopo la majadiliano; wakati akijibu maswali mbalimbali ya washiriki amesema TIRA ina vipaumbele mbalimbali mojawapo kikiwa ni kuongeza utoaji elimu kwa wananchi ili kuongeza uelewa wa bima kwa 80% ifikapo mwaka 2030, kundi la wanawake pia likiwemo.

Kwa upande mwingine wazungumzaji mbalimbali wamechangia nafasi ya mwanamke katika ujumuishi wa kifedha ni pamoja na Mhe. Saada Mkuya Waziri Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar, Naibu Kamishna wa Bima Bi. Khadija Said, Naibu Gavana Utawala na Udhibiti wa Ndani Benki Kuu Dkt. Rahma Salim Mahfoudh pamoja na wadau wengine mbalimbali kutoka sekta ya fedha.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA