Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Mkutano wa Baraza TIRA: Dkt. Saqware ahimiza watumishi kuzingatia vipaumbele vya Taasisi
10 Feb, 2026
Mkutano wa Baraza TIRA: Dkt. Saqware ahimiza watumishi kuzingatia vipaumbele vya Taasisi

Leo Februari 10, 2026 Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeendelea na Kikao cha Pili na Mkutano wa Nne wa Baraza la Nne la Wafanyakazi wa TIRA hapa katika ukumbi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani Pwani ambapo Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye ni Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware,amesisitiza Watumishi kuzingatia vipaumbele vya Taasisi.

Aidha, ameeleza uzingatiaji huo utafanikisha utekelezaji wa malengo makubwa ya kitaifa na ya Serikali kwa jumla, hususan katika kuimarisha mchango wa sekta ya bima katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya taifa letu.

Kwa upande mwingine,kikao hicho kimewakutanisha watumishi wa TIRA kutoka kada mbalimbali kwa lengo la kujadili masuala ya ustawi wa watumishi, utekelezaji wa majukumu ya taasisi pamoja na namna bora ya kuimarisha utendaji kazi ili kufikia malengo ya taasisi, sekta ya bima na Taifa kwa ujumla.

Akifunga Kikao hicho Dkt. Saqware amewasihi watumishi wa TIRA kuendelea kujituma na kufanya kazi kwa weledi  unaowiana na malengo ya taasisi, sekta ya bima pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na TIRA itaendelea kuhakikisha inahudumia wateja wa bima kwa viwango vinavyoakisi ubora wa mdhibiti, kwa kusimamia kwa ufanisi shughuli za bima nchini, kulinda haki za wateja wa bima na kuimarisha uimara na ustahimilivu wa sekta ya bima.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA