Kuelekea Siku ya Bima Tanzania Juni 20, 2025: Fahamu mambo muhimu yatakayofanyika na Jisajili kupitia www.iit.co.tz

Kuanzia Juni 19 – Juni 21 2025, itakuwa ni wiki yenye kuacha historia katika sekta ya bima kwa mwaka 2025, kwakuwa matukio mbalimbali kuhusu bima yatafanyika kama kielelezo cha kuonyesha uwajibikaji katika ukuzaji wa sekta hiyo. Sasa ni zamu ya Arusha, ambapo matukio yote yatafanyika hapo.
Matukio hayo ni kama Urudishaji kwa Jamii (Community Social Responsibility) ambapo wadau mbalimbali katika sekta ya bima watatoa msaada katika shule ya Mount Meru jijini Arusha Juni 18, 2025. Bima Walk tarehe 19 Juni 2025, matembezi maalumu ya kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa bima na matumizi ya bima. Matembezi hayo yataanzia eneo la uwanja wa mgambo. Tarehe 20, Juni 2025 itakuwa ni kilele cha Siku ya Bima ambapo utafanyika mkutano mkuu wenye matukio mbalimbali kama majadiliano na hotuba za viongozi.
Mkutano Mkuu utafanyika katika hoteli ya Gran Melia iliyopo Simeon Road, Arusha 1184. Viongozi mbalimbali wa Serikali watashiriki akiwemo Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware pamoja na viongozi na watumishi wa Mamlaka.
Siku ya Bima Tanzania imeandaliwa na Taasisi ya Bima Tanzania IIT kwa kushirikiana na TIRA na wadau wengine katika sekta. Ili kushiriki jisajili kupitia www.iit.co.tz