Kuelekea Saba Saba 2025: "Maonesho haya ni Fahari ya Tanzania" – Mhe. Chalamila. TIRA Tunashiriki

Hayo yamesemwa leo Juni 26, 202 na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila wakati wa hotuba yake kama mgeni rasmi katika semina maalumu ya maandalizi ya Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Saba Saba (Pre Fair Seminar) katika ofisi za TANTRADE zilizopo viwanja vya Saba Saba Dar es Salaam ambapo wadau wa Ofisi za Serikali, Taasisi na kampuni binafsi wameshirika, ambapo TIRA TUNASHIRIKI.
Aidha alieleza Maonesho hayo ni kielelezo cha diplomasia kwasababu mataifa mbalimbali yatashiriki na kutoa rai kwa wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla kushiriki kwa kuuza na kununua bidhaa mbalimbali.
Kwa upande wake, Bi. Latifa M. Khamis Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE amesema Maonesho ya mwaka huu ni ya tofauti kwani yapo kidigitali katika maeneo mbalimbali kama ununuzi wa tiketi lakini pia urahisishwaji wa usafiri kufikia mabanda umeboreshwa.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imejipanga kikamilifu kushiriki ambapo ‘Kijiji cha Bima’ kitakuwa na kampuni mbalimbali za bima pamoja na banda la NHIF kutoa huduma mbalimbali za bima zikiwemo bima za vyombo vya moto, bima za afya, bima za kilimo, bima za maisha na nyinginezo.
Njoo Kijiji cha bima upate elimu ya bima,utoe maoni lakini pia upate bima yako kwa kinga ya mali na uwekezaji. Maonesho yataanza rasmi Jumamosi, Juni 28 2025 hadi Julai 13 2025.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA