Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Kuelekea kuwa na Ithibati ya Ubora: Mafunzo ya Mfumo wa Ubora (QMS) yaendelea TIRA 
10 Mar, 2026
Kuelekea kuwa na Ithibati ya Ubora: Mafunzo ya Mfumo wa Ubora (QMS) yaendelea TIRA 

Kuelekea kuwa na Ithibati ya Ubora: Mafunzo ya Mfumo wa Ubora (QMS) yaendelea TIRA 

Je, Taasisi inawezaje kuhakikisha  huduma zake zinatolewa kwa ubora unaokubalika kimataifa? Hili ndilo lengo linalosukuma juhudi za Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) katika kuimarisha Mfumo wa Usimamizi wa Ubora (QMS). Watumishi wa TIRA ambao ni watekelezaji wa mfumo huo wanaendelea na mafunzo yanayofanyika TIRA Bima House, Njedengwa, Dodoma kuanzia tarehe 9 hadi 13 Machi 2026, yakilenga kuwajengea uwezo kwa ajili ya utekelezaji wa viwango vya ubora vya ISO ndani ya taasisi.

Kupitia mafunzo hayo, washiriki wanapatiwa uelewa wa taratibu za utekelezaji wa mfumo wa ubora pamoja na majukumu yao katika kuhakikisha mifumo na michakato ya kazi (work processes) inazingatia viwango vinavyotakiwa.

Kwa sasa mafunzo yanaelekezwa zaidi kwenye mada ya ukaguzi wa ndani wa mfumo wa ubora (Internal Quality Audit), ambapo washiriki wanajifunza namna ya kufanya ukaguzi wa michakato ya kazi na kubaini maeneo yanayohitaji maboresho jambo litalosaidia upatikanaji wa huduma bora kwa wadau na wananchi kwa jumla.

Kwa ujumla, Mfumo wa Usimamizi wa Ubora (QMS) una umuhimu mkubwa kwa TIRA kwani unasaidia kuboresha utoaji wa huduma, kuimarisha uwajibikaji na kuhakikisha taasisi inafanya kazi kwa ufanisi kulingana na viwango vya kimataifa.Mafunzo hayo yanaratibiwa na kitengo cha Udhibiti Ubora na Vihatarishi (QRM).

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA