Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Kuelekea kupata Ithibati ya Kiwango cha ISO 9001:2015; TIRA yawajengea uwezo watekelezaji wa mfumo wa ubora
20 Feb, 2026
Kuelekea kupata Ithibati ya Kiwango cha ISO 9001:2015; TIRA yawajengea uwezo watekelezaji wa mfumo wa ubora

Kuelekea kupata Ithibati ya Kiwango cha ISO 9001:2015; TIRA yawajengea uwezo watekelezaji wa mfumo wa ubora

Kuelekea utekelezaji wa mpango kazi unaolenga kupata ithibati ya kiwango cha ISO 9001:2015; Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), kupitia Kitengo cha Usimamizi wa Ubora na Hatari (QRM), imeendelea kutoa mafunzo kwa watumishi wanaotekeleza Mfumo wa Usimamizi wa Ubora (QMS Implementers).

Mafunzo hayo ya siku tano yameanza tarehe 16 Februari 2026 na kuhitimishwa leo tarehe 20 Februari 2026 katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya TIRA jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kutekeleza matakwa ya kiwango hicho cha kimataifa.

Aidha, mafunzo hayo yametolewa na wawezeshaji kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS), ambapo leo washiriki wamefanya mtihani wa kujipima uliodumu kwa saa mbili. Washiriki watakaofaulu mtihani huo wataendelea na hatua zinazofuata, ikiwemo kushiriki mafunzo ya Ukaguzi wa Kiwango cha ISO 9001:2015 yanayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 02 hadi 06 Machi 2026 katika Ofisi za TIRA Bima House – Njendegwa, Dodoma.

Hatua hii inaendelea kuimarisha uwezo wa ndani wa taasisi katika kuhakikisha utekelezaji madhubuti wa Mfumo wa Usimamizi wa Ubora, sambamba na kuboresha utoaji wa huduma kwa wadau wa sekta ya bima nchini.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA