The United Republic of Tanzania

Tanzania Insurance Regulatory Authority

“TIRA kwa Soko Salama la Bima”
Kikao cha Tano cha Wafanyakazi TIRA: Dkt. Saqware aeleza mafanikio thabiti Sekta ya Bima
01 Aug, 2026
Kikao cha Tano cha Wafanyakazi TIRA: Dkt. Saqware aeleza mafanikio thabiti Sekta ya Bima

Kamishna wa Bima, Dkt. Baghayo Saqware, ameeleza mafanikio thabiti ambayo yamepatikana katika sekta ya bima wakati wa Kikao cha Tano cha wa Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) unaofanyika katika Hoteli ya Eden Highland, jijini Mbeya, leo tarehe 30 Julai 2026 ambapo ni Mgeni Rasmi.

Kikao cha Tano kinalenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Mwaka wa Fedha 2025/2026 pamoja na Mpango Mkakati wa Sita wa TIRA kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027. Aidha, unatoa fursa ya kujadili vipaumbele vya Mamlaka, kutathmini utekelezaji wake na kusikiliza maoni ya watumishi kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo yao na taasisi kwa jumla.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao hicho, Dkt. Saqware amesema mafanikio thabiti yameonekena sekta ya bima na imeendelea kukua kwa kasi, akibainisha kuwa idadi ya watoa huduma za bima imeongezeka kutoka 800 mwaka 2019 hadi 2,444 mwaka 2025. Vilevile, watumiaji wa huduma za bima wameongezeka kutoka asilimia 8.4 mwaka 2019 hadi asilimia 38.6 mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 30 ndani ya kipindi cha miaka mitano.

Pia amesema ajira rasmi katika sekta ya bima zimeongezeka kutoka 3,189 mwaka 2019 hadi 7,206 mwaka 2025. Aidha, mchango wa sekta ya bima katika Pato la Taifa (GDP) umeongezeka kutoka asilimia 1.55 mwaka 2019 hadi asilimia 2.11 mwaka 2025, huku TIRA ikiendelea kuweka mikakati ya kufikisha mchango huo hadi asilimia 5 ifikapo mwaka 2050.

Kwa upande mwingine, Dkt. Saqware amewahimiza watumishi wa TIRA kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, weledi na uzalendo ili kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wadau na wananchi, kufanikisha malengo ya Mamlaka na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo.

1d