The United Republic of Tanzania

Tanzania Insurance Regulatory Authority

“TIRA kwa Soko Salama la Bima”
TIRA yang’ara Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki Mwanza
04 Sep, 2026
TIRA yang’ara Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki Mwanza

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima - TIRA imeibuka kinara na kuwa mshindi wa kwanza miongoni mwa taasisi za umma zinazoshiriki katika maonesho ya 21 ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Furahisha, Ilemela, Mwanza.

Tuzo hiyo imekabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade Bw. Ephraim Balozi Mafuru, ambaye amesisitiza  taasisi za umma kushiriki maonesho mbalimbali ili kufikisha huduma za Serikali karibu na wananchi.

Meneja wa TIRA Kanda ya Ziwa, Bw. Phostine Oyuke, ametoa wito kwa wananchi kutumia fursa ya maonesho hayo kutembelea banda la TIRA ili kupata elimu na ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya bima yakiwemo fursa zilizopo katika soko la bima, pamoja na haki zao kama watumiaji wa huduma za bima, hususan katika masuala ya madai.

Maonesho hayo ambayo yameanza tarehe 28 Agosti na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 6 Septemba 2026, yamenatoa fursa kwa wananchi na wadau mbalimbali kujifunza umuhimu na fursa za bima katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii. 

TIRA Kwa Soko Salama la Bima