Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware Ahudhuria Kikao cha Kwanza cha Baraza la Usalama Barabarani
Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware Ahudhuria Kikao cha Kwanza cha Baraza la Usalama Barabarani
Dodoma – Kamishna wa Bima, Dkt. Baghayo Saqware, leo tarehe 16 Mei 2026 amehudhuria Kikao cha kwanza cha Baraza la Usalama Barabarani kilichofanyika jijini Dodoma chini ya uongozi wa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo.
Akizungumza wakati wa utambulisho wa wajumbe, Mhe. Naibu Waziri alimpongeza Dkt. Saqware kwa mchango wake mkubwa katika awamu iliyopita, akisisitiza kuwa sekta ya bima imekuwa na sauti madhubuti katika masuala ya usalama barabarani. Aidha, alieleza matarajio makubwa aliyonayo kwake katika awamu hii mpya ya baraza.
Dkt. Saqware ambae anahudumu kwenye Baraza la Usalama Barabarani kwa kipindi cha pili mfululizo ameahidi kuendeleza ushirikiano katika kuiwakilisha vyema sekta ya bima ambae ni mdau mkubwa wa maswala ya usalama barabaranj.
Katika kipindi kilichopita Dkt. Saqware ameiwakilisha vyema sekta ya bima kwa kupeleka mbele ajenda muhimu zinazohusu bima za vyombo vya moto. Lengo kuu ni kuhakikisha wananchi wanapata unafuu wa haraka na uhakika wanapokumbwa na majanga barabarani napia watumiaji na wamiliki wa vyombo vya moto kuzingatia Sheria ya bima za vyombo vya moto wakati wote.
Ushiriki wake unaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya bima na serikali katika jitihada za kupunguza athari za ajali na kuboresha usalama kwa watumiaji wote wa barabara na vyombo vya moto.
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ni chombo kilichoundwa kwa mujibu wa sheria ya usalama barabarani kwa lengo la kusimamia, kuratibu na kuendeleza maswala yanayohusu usalama barabarani nchini.
