Dkt. Saqware: Sekta Imara ya Bima ni chachu ya Utekelezaji Dira 2050
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imesema sekta imara na endelevu ya bima ni chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku ikizitaka Kampuni za Bima kuwa na mitaji imara, kukua, kupata faida na kutoa huduma bora kwa Watanzania.
Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware, wakati wa ziara ya kimkakati ya TIRA katika Kampuni za Bima, ikiwemo ICEA LION (Simba wa Bima), inayofanyika Agosti 12–14, 2026.
Dkt. Saqware amesisitiza umuhimu wa kampuni za bima kuimarisha mitaji, uwekezaji, matumizi ya teknolojia na ubunifu wa bidhaa na huduma, pamoja na kudhibiti udanganyifu katika soko la bima.
Amesema TIRA itaendelea kushirikiana na Kampuni za Bima na kuboresha mazingira ya udhibiti ili kukuza sekta, kuongeza upatikanaji wa huduma za bima na kuchangia ajira, uwekezaji na maendeleo ya Taifa.
“Tunaamini tukitekeleza Dira 2050 tutakuwa na Taifa linaloweza kutatua changamoto zinazozunguka maisha ya Watanzania kupitia huduma za bima,” alisema Dkt. Saqware.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imesema sekta imara na endelevu ya bima ni chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku ikizitaka Kampuni za Bima kuwa na mitaji imara, kukua, kupata faida na kutoa huduma bora kwa Watanzania.
Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware, wakati wa ziara ya kimkakati ya TIRA katika Kampuni za Bima, ikiwemo ICEA LION (Simba wa Bima), inayofanyika Agosti 12–14, 2026.
Dkt. Saqware amesisitiza umuhimu wa kampuni za bima kuimarisha mitaji, uwekezaji, matumizi ya teknolojia na ubunifu wa bidhaa na huduma, pamoja na kudhibiti udanganyifu katika soko la bima.
Amesema TIRA itaendelea kushirikiana na Kampuni za Bima na kuboresha mazingira ya udhibiti ili kukuza sekta, kuongeza upatikanaji wa huduma za bima na kuchangia ajira, uwekezaji na maendeleo ya Taifa.
“Tunaamini tukitekeleza Dira 2050 tutakuwa na Taifa linaloweza kutatua changamoto zinazozunguka maisha ya Watanzania kupitia huduma za bima,” alisema Dkt. Saqware.
