Bima na Afya: TIRA yashiriki CRDB Marathon Dar es Salaam
17 Aug, 2026
Agosti 16, 2026
Haikuwa asubuhi kama nyingine! Ilikuwa asubuhi ya shamrashamra, furaha na hamasa, ambapo watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) waliungana na Watanzania mbalimbali kushiriki katika mbio za CRDB Marathon.
TIRA imeshiriki katika mbio hizo kwa dhamira ya kuhamasisha watumishi kuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi na kuzingatia afya na ukakamavu mahali pa kazi.
Aidha, watumishi walibeba mabango mbalimbali yenye jumbe za TIRA ili kuleta uelewa zaidi kwa Wananchi kuhusu shughuli za TIRA.
#Bima na afya kwanza
#TIRA kwa soko salama la Bima
