Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Kamishna wa Bima apongeza kuanzishwa kwa 'Mufti Bima Faundation'
08 May, 2026
Kamishna wa Bima apongeza kuanzishwa kwa 'Mufti Bima Faundation'

Kamishna wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt. Baghayo Saqware ameshiriki uzinduzi wa Taasisi ya Mfuko wa Bima ya Afya wa Mufti ijulikanayo kama Mufti Bima Foundation, yenye lengo la kusaidia Watanzania wenye mahitaji maalum kumudu gharama za matibabu.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika leo Mei 7, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi Kuu ya BAKWATA jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Bima nchini, amepongeza BAKWATA kwakuanzisha mfuko huo, akieleza kuwa hatua hiyo inaunga mkono juhudi za Serikali katika kufanikisha huduma ya Bima ya Afya kwa Wote nchini.

Dkt. Saqware amesema TIRA, kama msimamizi wa sekta ya bima nchini, inatambua kuwa kuanzishwa kwa mfuko huo ni matokeo ya maono ya Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma za bima ya afya.

Aidha, amempongeza Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa akiwa ndiye mgeni rasmi katika uzinduzi huo kwa mchango wake mkubwa katika kutoa mwelekeo wa utekelezaji wa ajenda ya Bima ya Afya kwa Wote, akibainisha kuwa, hatua ya BAKWATA chini ya uongozi wa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuber Ali Mbwana ni sehemu ya kuisaidia Serikali kufikia malengo hayo.

TIRA, Kwa Soko Salama la Bima.