Huduma bora za bima kwa Wananchi; Waziri wa Fedha azindua mikakati muhimu sekta ya bima
Huduma bora za bima kwa Wananchi; Waziri wa Fedha azindua mikakati muhimu sekta ya bima
Leo Aprili 9, 2026 Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar amezindua rasmi Mikakati miwili muhimu katika uendelezaji sekta ya bima kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA); ukiwemo Mkakati wa Kitaifa wa Huduma za Bima Jumuishi 2025-2030 (NIIS) na Mkakati wa Kitaifa wa Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji Soko la Bima, 2025 – 2030 (RIDeS). Uzinduzi huo umefanyika katika Jukwaa la Wadau Sekta ya Fedha 2026 katika ukumbi wa PSSSF Commercial Complex jijini Dar es Salaam.
Waziri ameipongeza TIRA kwa mikakati hiyo ambayo inaongeza chachu ya ukuaji jumuishi katika sekta ya Fedha lakini pia inatoa wigo mpana wa utafiti na ubunifu katika maeneo mbalimbali ya sekta ya bima mathalani fursa katika bima inayofata misingi ya kisheria – Takaful.
Aidha, Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware akitoa ufafanuzi mfupi wa mikakati hiyo ameeleza Mkakati wa Kitaifa wa Huduma za Bima Jumuishi 2025-2030 (NIIS) unalenga kuongeza upatikanaji wa huduma za bima katika maeneo muhimu kama kilimo, ufugaji, uvuvi, madini na misitu, ujumuishaji wa kifedha katika huduma za bima huku Mkakati wa Kitaifa wa Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji Soko la Bima, 2025 – 2030 (RIDeS) unalenga kuongeza ubunifu, ufanisi na ukuaji katika sekta ya bima.
Jukwaa hilo limehudhuriwa na wadau mbalimbali katika sekta ya fedha na kwa upande wa sekta ya bima kampuni za bima, madalali wa bima, benkiwakala wa bima na mawakala wa bima wameshiriki.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA
