Bima ni Mkakati wa Kujiandaa dhidi ya Majanga asema Mchengerwa...Kamishna wa Bima apigia chapuo (aunga mkono)
Waziri wa Afya nchini Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa msisitizo kwa wahariri kuwa Bima ni mkakati madhubuti dhidi ya majanga yakiwemo maradhi hivyo kuwataka wanahabari hao kupeleka elimu hiyo kwa wananchi ili waweze kuelewa vyema na hatimaye kujiunga na mfumo wa bima.
Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo leo, Februari 2, 2026, jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi maalum na wahariri kuhusu utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote. Amesema wanahabari wana nafasi kubwa ya kuhakikisha wananchi wanapata uelewa sahihi kuhusu mfumo wa bima ya afya ili hatimaye waweze kujiunga na kunufaika na huduma hiyo muhimu.
Kwa upande wa Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware wakati wa wasilisho lake kuhusu majukumu ya TIRA katika usimamizi wa bima ya afya kwa wote ameahidi ushirikiano wa Mamlaka kwa wanahabari katika kupata taarifa sahihi kuhusu bima ya afya kwa wote na kuunga mkono kauli ya Mhe. Mchengerwa kwamba bima ni mkakati wa kujiandaa dhidi ya majanga yasiyotarajiwa.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA
