The United Republic of Tanzania

Tanzania Insurance Regulatory Authority

“TIRA kwa Soko Salama la Bima”
Wananchi wapongeza huduma za bima kilele cha Maonesho ya Saba Saba 2026
07 Jul, 2026
Wananchi wapongeza huduma za bima kilele cha Maonesho ya Saba Saba 2026

Leo tarehe 7 Julai 2026, ikiwa ni kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara Saba Saba wananchi mbalimbali wamepongeza uwepo wa Kijiji cha Bima baada ya kupata elimu ya bima lakini pia kuhudumiwa na watoa huduma za bima zaidi ya 40 waliopo ndani ya Kijiji hicho.

Akieleza baada ya kupata elimu ya bima kutoka banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Bw. Kelvin K. Msuya mkazi wa Temeke Dar es Salaam ameshukuru kwa kupata elimu hiyo na pia kufahamu kuhusu aina za bima mbalimbali ikiwemo bima ya maisha ulikilinganisha na bima chache alizofahamu awali.

Kwa upande mwingine Bi. Salma Hamza mkazi wa Kibaha Pwani ameeleza kufurahishwa na huduma za Bima zinazofuata misingi ya kidini – Takaful lakini pia bima za usafirishaji ambazo amekutana na kampuni husika ili aweze kuzitumia katika shughuli za biashara zake.

Wananchi wote mnakaribishwa katika banda la Kijiji cha Bima katika Maonesho ya Saba Saba ambapo yatahitimishwa rasmi tarehe 13 Julai, 2026.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA