TIRA YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA KITAIFA
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) leo tarehe 25 Julai 2026 imeshiriki kuadhimisha Kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa katika hafla ya kitaifa ambayo imefanyika katika Viwanja vya Mashujaa, Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Maadhimisho hayo yameongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kuhudhuriwa na viongozi wakuu wa Serikali, vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ambapo pia watumishi kutoka TIRA wameshiriki wakiongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Nakaunda Mangosongo.
Aidha, Siku ya Mashujaa pia imehudhuriwa na viongozi na washiriki walishiriki katika shughuli mbalimbali za kutoa heshima kwa mashujaa wa Taifa, ikiwemo uwekaji wa mashada ya maua kwenye Mnara wa Mashujaa, gwaride la maombolezo, upigaji wa mizinga ya heshima pamoja na ukimya wa dakika moja kwa ajili ya kuwaenzi wale waliojitolea maisha yao katika kulinda uhuru, amani na umoja wa Tanzania.
Ushiriki wa TIRA katika maadhimisho hayo unaonesha dhamira ya kuenzi historia ya Taifa, kuthamini mchango wa mashujaa waliopigania uhuru na kudumisha maadili ya uzalendo, uwajibikaji na huduma kwa wananchi. Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa hufanyika tarehe 25 Julai kila mwaka.
