TIRA yashiriki uzinduzi wa Polisi Jamii Cup Rufiji 2026
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeshiriki katika uzinduzi wa Mashindano ya Polisi Jamii Cup Mkoa wa Kipolisi Rufiji 2026, yaliyofanyika tarehe 3 Septemba 2026 wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani. Mashindano hayo yamezinduliwa rasmi na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Camillus Wambura; ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na jamii kupitia michezo.

TIRA imeshiriki katika tukio hilo kupitia Kanda ya Mashariki, inayojumuisha Dar es Salaam, Morogoro na Pwani, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Mamlaka za kuendelea kujenga na kuimarisha mahusiano mema na Jeshi la Polisi pamoja na kushirikiana katika masuala yenye maslahi kwa jamii.
Katika uzinduzi huo, TIRA imewakilishwa na Meneja wa TIRA Kanda ya Mashariki, Bw. Kurenje Mbura, kwa niaba ya Kamishna wa Bima. Ushiriki huo unaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya TIRA na Jeshi la Polisi, hususan katika kufikisha elimu kwa jamii kuhusu masuala ya bima na usalama barabarani.

Aidha, TIRA imedhamini Mashindano ya Polisi Jamii Cup Rufiji 2026 kwa kutoa jezi za michezo, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Jeshi la Polisi katika kuimarisha mahusiano na jamii kupitia michezo. Kupitia ushiriki huo, TIRA pia inatumia fursa hiyo kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuzingatia usalama barabarani, ikiwemo matumizi sahihi ya barabara na kuchukua tahadhari zinazosaidia kupunguza ajali.
#Bima na Usalama Barabarani
#TIRA kwa Soko Salama la Bima
