PIC yaridhishwa na ukuaji wa Sekta ya Bima nchini
PIC YARIDHISHWA NA UKUAJI WA SEKTA YA BIMA NCHINI
DODOMA, Agosti 20, 2026 -
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma PIC imeridhishwa na maendeleo ya sekta ya bima nchini, ikiipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA kwa kazi kubwa ya kuongeza ufikiaji na ufanisi wa huduma.
Hayo yamebainishwa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, *
Mhe. Masanja Kadogosa mara baada ya kupokea wasilisho kutoka kwa Kamishna wa Bima, Dkt. Baghayo Saqware kwenye kikao cha PIC na TIRA.
Mhe. Kadogosa amesema ukuaji huo umechangiwa na kuongezeka kwa uelewa wa bima miongoni mwa wananchi hivyo kusababisha idadi ya watumiaji kuongezeka.
“Tunaipongeza TIRA. Tunaomba muendelee kutoa elimu ya bima kwa kutumia njia za kibunifu ili kufikia Watanzania wengi zaidi” amesema Kadogosa.
Kwa upande wake, Mhe. Twaha Mwakioja Mjumbe wa PIC ameiagiza TIRA kuimarisha usimamizi wa sheria na miongozo ya bima ili kuhakikisha kampuni zote zina mitaji ya kutosha ili kuhakikisha fidia za wananchi zinalipwa kwa wakati iwapo kutatokea majanga.
Akitoa wasilisho lake, Dkt. Saqware ameeleza kuwa soko la bima limeendelea kukua kwa kasi huku akitaja baadhi ya sababu kuwa ni juhudi za serikali kupitia Wizara ya Fedha kwa kuweka mazingira wezeshi ya utendaji kazi kupitia sheria na miongozo mbalimbali ambayo imewezesha usimamizi madhubuti wa TIRA kwa sekta ya bima kupitia ofisi na kanda zake Kumi zinazohudumia mikoa yote nchini.
Dkt. Saqware ameendelea kubainisha kuwa ulipaji wa madai umeongezeka kwa 57% mwaka 2025 ikilinganishwa na meaka 2023 na hivyo kuongeza imani ya wananchi kuhusu huduma za bima.
Ameeleza pia mifumo ya TEHAMA kama vile TIRAMIS, TIRA-ORS, TSS Portal na IRIS imeimarika smbapo imerahisisha utoaji wa leseni, malipo ya ada za bima na kuongeza uwazi, ufanisi na kasi ya utoaji huduma.
