The United Republic of Tanzania

Tanzania Insurance Regulatory Authority

“TIRA kwa Soko Salama la Bima”
TIRA yaunga Mkono Polisi Jamii Cup 2026 Rufiji, yasisitiza Usalama Barabarani
29 Aug, 2026
TIRA yaunga Mkono Polisi Jamii Cup 2026 Rufiji, yasisitiza Usalama Barabarani

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imetoa msaada wa jezi kwa ajili ya mashindano ya Polisi Jamii Cup 2026 yanayotarajiwa kufanyika mapema Septemba 2026; wilayani Rufiji mkoa wa Pwani ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano na Jeshi la Polisi katika shughuli za kijamii na uhamasishaji wa usalama barabarani.

Aidha, Leo tarehe 28 Agosti 2026; SACP Protas Mutayoba, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji (RPC) pamoja na maafisa wengine wa Jeshi la Polisi wamefanya kikao cha kimkakati na Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware katika Ofisi za TIRA, Dar es Salaam lengo likiwa ni kujadili na boresha mahusiano lakini pia kutoa shukrani kwa msaada huo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Saqware, amesema TIRA itaendelea kudhamini mashindano hayo na kuwa karibu na Jeshi la Polisi, hususan katika masuala yanayohusu usalama barabarani, pia amesisitiza kuwa TIRA itashiriki katika mashindano hayo yatakayofanyika mwanzoni mwa mwezi Septemba 2026.

Kwa upande wake, RPC Rufiji amesema TIRA na Jeshi la Polisi ni wadau wakubwa katika masuala ya usalama barabarani na kuishukuru TIRA kwa msaada huo huku akieleza kuwa Polisi Jamii Cup ni fursa muhimu ya kuhamasisha usalama katika jamii, hususan kwa kundi la waendesha bodaboda.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA