Kigoma: TIRA Yaweka Mkazo kwenye Elimu ya Bima katika Lake Tanganyika International Expo
20 Sep, 2026
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) inaendelea kushiriki katika Maonesho ya Biashara na Uwekezaji ya Lake Tanganyika International Expo yanayofanyika katika viwanja vya Mwanga Community City, mkoani Kigoma, kwa kutoa elimu kuhusu bima na nafasi ya sekta hiyo katika shughuli za kiuchumi.

Kupitia banda lake, TIRA inaendelea kuwafikia wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji wanaotembelea maonesho hayo, ambapo wanapata elimu kuhusu aina mbalimbali za bima, umuhimu wa kuwa na kinga ya bima pamoja na namna huduma za bima zinavyoweza kusaidia kulinda biashara, mali na shughuli za uzalishaji dhidi ya vihatarishi mbalimbali.
Aidha, wananchi wanaelezwa kuhusu majukumu ya TIRA katika kusimamia na kuendeleza sekta ya bima nchini, pamoja na fursa zinazopatikana katika sekta hiyo, ikiwemo kuanzisha biashara zinazohusiana na bima na kufanya shughuli za uwakala wa bima.
_1789899552.jpeg)
