Waziri Riziki apongeza TIRA kwa utoaji elimu - Maadhimisho Miaka 62 ya Muungano
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Riziki Pembeni Juma, ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kwa juhudi zake endelevu za kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya bima nchini.
Ametoa pongezi hizo leo Aprili 26, 2026, alipofanya ziara katika banda la TIRA wakati wa Maadhimisho ya Miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na mamlaka hiyo.
Katika ziara hiyo, Waziri Riziki aliambatana na viongozi mbalimbali, huku wakipata maelezo ya kina kuhusu mwenendo wa soko la bima nchini, umuhimu wake kwa wananchi pamoja na aina tofauti za huduma za bima zinazopatikana.
Maadhimisho hayo yaliyoanza Aprili 21, 2026, yamehitimishwa rasmi leo, ambapo Dkt. Riziki Pembeni Juma alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kufunga maonesho hayo.
