Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Tunatekeleza: Mamlaka yakutana na watoa huduma za bima Kanda ya Magharibi
06 Jun, 2025
Tunatekeleza: Mamlaka yakutana na watoa huduma za bima Kanda ya Magharibi

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kupitia kanda ya Magharibi inayohudumu mikoa ya Tabora, Shinyanga na Singida imekutana na watoa huduma za bima wa kanda hiyo tarehe 03 Juni 2025 katika ofisi za Mamlaka mkoani Tabora. Lengo likiwa kukumbushana masuala mbalimbali katika sekta ya bima.

Meneja wa Kanda hiyo Dkt. Emmanuel Lupilya wakati wa ufunguzi wa mkutano huo alieleza lengo la kukutana ni kukumbushana uwajibikaji na ufanisi katika utoaji huduma, umuhimu wa uandikishaji biashara, uzingatiaji wa miongozo, matumizi ya mabango sahihi yaliyowekwa na Mamlaka lakini pia kuongeza fursa na uandikishaji wa bima.

Vilevile, Meneja Lupilya pia alisisitiza juu ya umoja kwa wasajiliwa hao kama chanzo cha ukuzaji wa huduma na pia kueleza ushirikishwaji wa wadau hao katika utoaji elimu ya bima ili kuongeza uelewa na matumizi ya bima nchini.

Ofisi za TIRA mkoani Tabora zipo TUWASA Barabara ya boma, mtaa wa Gongoni. Karibu sana tupo kukusikiliza.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA