TIRA yatoa elimu ya bima Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kupitia kanda ya kati, Dodoma imetoa elimu ya bima kwa wanachuo wa Chuo cha Serikali za Mitaa kilichopo Hombolo Mei 20, 2025 jijini Dodoma. Elimu hiyo ililenga kuwawezesha wanafunzi kuelewa dhana ya bima, aina mbalimbali za bima, umuhimu wa kuwa na bima, pamoja na majukumu ya TIRA katika kusimamia sekta ya bima nchini.
Aidha, wanachuo hao walipata fursa ya kuuliza maswali na kushiriki katika majadiliano kuhusu mafanikio na changamoto wanazoziona katika masuala ya bima na pia kueleza namna watakavyoweza kusambaza elimu hiyo kwa watu hao wa karibu ii waweze kutumia huduma za bima kujikinga na majanga mbalimbali.
Zaidi kupitia elimu hii, TIRA inaendelea kutekeleza jukumu lake la kuelimisha umma kuhusu bima kwa mujibu wa Mpango Mkakati wa Mamlaka (CSP), ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupanua uelewa na wigo wa soko la bima nchini.
Pia, Ofisi za TIRA kanda ya kati zipo jijini Dodoma, mtaa wa Makole jengo la PSSSF House ghorofa ya 5 na kanda hii pia inahudumia mikoa ya Iringa na Manyara katika kutekeleza majukumu yake.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA