Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha afungua rasmi Mkutano wa TUGHE Tawi la TIRA
18 Mar, 2026
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha afungua rasmi Mkutano wa TUGHE Tawi la TIRA

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha afungua rasmi Mkutano wa TUGHE Tawi la TIRA

Mshikamano! 
Kama ilivyo salamu rasmi inayoashiria umoja ndani ya Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania – TUGHE, leo Machi 18, 2026 salamu hiyo; “Mshikamano” imejidhihirisha wazi kwa wanachama wa Tawi la TIRA kukutana na kupeana taarifa mbalimbali kwa ustawi wa wanachama katika Mkutano unaoendelea hapa Kibaha, Pwani.

Aidha, Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Nickson Simon John ambaye amepongeza TIRA kwa kuwa na chama (TUGHE) kinachozungumzia mambo mbalimbali ya watumishi lakini pia ametoa rai kwa uongozi; kutolewa kwa elimu zaidi ya umuhimu wa chama hicho ili kuongeza idadi ya wanachama na mwisho kabisa ametoa msisitizo kwa watumishi kuongeza ujuzi ili kuendana na kasi ya Teknolojia kama Akili Mnemba (AI) na kuboresha utendaji wa kazi na huduma kwa jamii. 

Vilevile, mkutano huo umetoa fursa ya kuwasilishwa kwa taarifa ya utendaji ya TUGHE – TIRA, pamoja na hapo baadae kutanyika uchaguzi wa viongozi wa nafasi mbalimbali. Mkutano huo pia umehudhuriwa na viongozi wa TUGHE Taifa. Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa TUGHE – TIRA, Bw. Sausi M. Sausi, amewahimiza wanachama kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA