Bima Walk yafana; wadau wa bima washiriki; Kuhamasisha matumizi ya bima

Matembezi ya kilometa tano za ushindi yalifanywa kwa moyo wa uhamasishaji lengo likiwa ni kuhamasisha matumizi ya bima nchini ambapo kwa mwaka huu ilikuwa zamu ya Arusha. Matembezi hayo yamefanywa na wadau mbalimbali wa bima leo tarehe 19 Juni 2025 na yalianza rasmi na kumalizikia viwanja vya Mgambo, Arusha.
Akitoa pongezi na shukrani Mkuu wa Wilaya Arusha Bw. Joseph Mkude, kama Mgeni Rasmi wa tukio hilo amewapongeza wadau walioshiriki na kupongeza Kamati kulichagua jiji hilo la kitalii kuhamaisha matumizi ya bima. Pia Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mawaziri Mhe. Injinia Zena Said aliungana na wadau kushiriki matembezi hayo kama Mgeni maalumu.
Aidha Bi. Hawa Mniga Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala kwa Niaba ya Kamishna wa Bima aliwapongeza washiriki wote na kusema matembezi hayo yameongeza chachu na ari katika matumizi ya bima jijini humo na jamii nzima kwa ujumla.
Matembezi hayo yalikuwa sehemu kuelekea Siku ya Bima Tanzania hapo kesho tarehe 20 Juni 2025.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA